Shamsa Ford Aiweka Rehani Ndoa Yake!
bonyeza hii picha hapa chini..kuona video ya shamsa
Katika mazungumzo na Star Mix msanii huyo mwenye uwezo wa ‘makinikia’ linapokuja suala la kuigiza, aliweka wazi kuwa kama mwanadamu haishiwi na mapungufu ambayo ameyatubu kwa Mungu.
“Kama binadamu siishiwi na makosa, lakini katika mfungo huu wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, yapo mengi ambayo niliyafanyia toba maalum, lakini kubwa sana ni uhai wa ndoa yangu, maana siko tayari kwa kweli kuvurugikiwa na kuvunjika kwa ndoa hii ambayo inamaanisha furaha ya maisha yangu, kwa hiyo naiweka ndoa yangu kwa Mungu na yote namuachia yeye,” alisema Shamsa.
Posted
at June 23, 2017,
Add Comment
Soma zaidi
Mambo 13 Nchi za Kiarabu zimeitaka Qatar itekeleze…moja ndani ya siku 10
Mtandao wa AL JAZEERA umeripoti leo June 23, 2017 kuwa nchi nne za kiarabu zikiongozwa na Saudi Arabia zimeipa Qatar masharti 13 ili kumaliza mgogoro uliopo baina yao ambapo moja katika masharti hayo ni kuitaka kukatisha mtandao wa Al Jazeera na kupunguza mahusiano na Iran.
Pia katika list hiyo, mataifa hayo yameitaka Qatar kutokuwa na mahusiano pia na makundi ya Muslim Brotherhood, Hezbollah, al-Qaeda na ISIL (pia hujulikana kama ISIS) wakiitaka pia kufunga kambi moja ya wanajeshi ya Uturuki ndani ya kipindi cha siku 10 pekee.
Nchi za Saudi Arabia, Misri, Falme za Kiarabu na Bahrain zilisitisha uhusiano wa kidiplomasia na Qatar mwezi huu kwa madai kuwa nchi hiyo inafadhili Ugaidi – madai ambayo Qatar inayapinga.
Posted
at June 23, 2017,
Add Comment
Soma zaidi
DALILI ZA KUKUONYESHA KUWA MAPENZI YA MWANAUME YAMEKWISHA KWAKO
Posted
at June 23, 2017,
Add Comment
Soma zaidi
Subscribe to:
Posts (Atom)